The House of Favourite Newspapers

Gomes: Nguvu Yetu Tutaionyesha Uwanjani

0

BIG bosi wa benchi la ufundi la Simba, Mfaransa Didier Gomes amebainisha wazi kwamba wataonyesha nguvu waliyonayo kwenye mechi yao ya marudiano dhidi ya Kaizer licha ya wengi kuwakatia tama.

 

Kocha huyo ameongeza kwamba anaamini wazi kwamba kikosi chake kinaweza kushinda mchezo huo wa marudiano na hapo ndipo wataonyesha juu ya nguvu ambayo wanayo kwenye michuano hiyo.

 

Simba watakuwa wenyeji wa Kaizer Chiefs katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika ambao utapigwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Mkapa, Dar.

Simba watalazimika kushinda mabao 5-0 kwa ajili ya kukata tiketi ya kuingia hatua ya nusu fainali baada ya kupoteza mchezo wa awali kwa mabao 4-0.

 

Gomes ameliambia Championi Jumatano, kuwa kwake bado hajakata tamaa kwani anaona wazi bado kuna nafasi ya timu yake kupata ushindi. “Tuna matumaini, tunaamini tunaweza kushinda kwenye mechi hii.

 

Tunahitaji kuweka nguvu na kuionyesha uwanjani, wachezaji wako vizuri na wana morali naamini juu ya hilo.”

Stori na Said Ally,Dar es Salaam

Leave A Reply