The House of Favourite Newspapers

LondonUpdates: Moto Wa Ghorofa La Grenfell Tower London Waua Watu 12 (Pichaz + Video)

0
Wafiwa na ndugu zao wakipewa pole na wananchi wa London.

WATU 12 wamethibitishwa kufa katika moto uliolitekeleza jengo la ghorofa 27 la Grenfell Tower jijini London, Uingereza, ambao ulilikumba tangu usiku wa kuamkia jana.  Vilevile makundi  kadhaa ya watu, wakiwemo watoto na wazee bado hawajulikani walipo katika jengo hilo la eneo la White City ambapo watu zaidi ya 79 walikimbizwa hospitali kwa matibabu.

Familia mbalimbali zikiwa nje ya baada ya makazi yao kuteketea kwa moto.

Ghorofa hilo ambalo lina wakazi 600 lilikumbwa na taharuki kubwa ambapo watu walijaribu kila njia kujiokoa na moto huo ambao ulianza usiku wa manane ambapo ving’ora vya kuashiria moto katika jengo hilo havikufanya kazi, vyombo maalum vya kunyunyiza dawa ya kuzima moto  navyo havikufanya kazi na njia maalum ya dharura ya kupita wakati wa majanga ya moto, ilikuwa imezibwa.

Hata hivyo, moto huo hatimaye ulifanikiwa kuzimwa jana na vikosi vya zimamoto na kuliacha jengo likiwa limeungua vibaya.

Watu walionusurika wakitafakari kilichotokea

Wataalam wa masuala ya moto wamesema kwamba wamiliki wa jengo hilo walikuwa walipewa onyo mara kwa mara kuhusu kuta zenye matabaka mbalimbali ambayo yangeweza kusababisha moto mdogo ukawa mkubwa.  Hata hivyo, inasemekana wamiliki hao hawauufanyia kazi ushauri huo.

Waokoaji wakiwa wamembeba mtu aliyepata madhara ya moto huo

Baadhi ya waliokumbwa na moto huo baada ya kuokolewa

Walioathirika na moto huo wakilia huku polisi wakifanya doria

Kikosi cha Zima Moto kikiwa kazini

Waathirika wa moto huo baada ya kuokolewa wakiwa na vifurushi walivyofanikiwa kuokoa

Baadhi ya watu waliookolewa

 

 

Binti aliyeokolewa akilia kwa uchungu baada ya kuokolewa, hapo anapiga simu kuwasiliana na ndugu zake

Jengo likiteketea kwa moto baada ya kukolea

Baadhi ya maiti zikiondolewa eneo la tukio

 

Leave A Reply