Henock Inonga Ashinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mashabiki wa Simba
HENOCK Inonga beki wa Klabu ya Simba leo amekabidhiwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mashabiki (Emirate Aluminium Simba ACP Fans Player of the Month) mwezi Aprili baada ya kuwashinda Shomari Kapombe na Joash Oyango ambao waliingia kwenye fainali.
Tuzo ambayo amepewa ni pamoja na mkwanja wa shilingi milioni mbili ambao ni zawadi yake beki huyo kitasa ambaye aliweza kuwka kwenye mchezo dhidi ya Yanga uliochezwa Aprili 30 kwa kumzuia Fiston Mayele kushindwa kufunga lango la Simba