The House of Favourite Newspapers

Hii Hapa Taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza

0
msangi
Tarehe 08.06.2016 majira ya saa 08:00hrs hadi saa 15:00hrs katika kisiwa cha Maisome kambi ya uvuvi migongo kata ya Maisome tarafa Kahunda  wilaya Sengerema  mkoa wa Mwanza, katika tukio la kwanza askari wakiwa doria  katika kisiwa tajwa hapo juu wakiambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Sengerema walifanikiwa kukamata nyavu (kokolo) haramu za kuvulia samaki 17 na timba 81 ambayo ni mitego ya kienyeji ya kutegea samaki, vilivyotelekezwa na wavuvi wasiojulikana  baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa askari wanaofanya doria na misako katika maeneo yao.
Jeshi la polisi linaendelea na misako pamoja na doria katika kisiwa hicho kwa kuhakikisha watuhumiwa waliotelekeza nyavu hizo haramu wanakamatwa na wengine wanaoshirikiana nao pia wanasakwa ili kukomesha uvuvi haramu katika kisiwa hicho, hii ni baada ya kupokea taarifa kutoka kwa raia wema kwamba katika kisiwa tajwa hapo juu kuna wavuvi ambao hutumia zana haramu katika shughuli zao za uvuvi za kila siku kitendo ambacho ni kinyume na sheria na taratibu za nchi.
Aidha tukio lingine sawa na tarehe na majiara tajwa  hapo juu kwenye kisiwa cha Kasarazi kata ya Bulyaheke tarafa ya Buchosa wilaya ya Sengerema, askari wakiwa doria walifanikiwa kukamata nyavu haramu za kuvulia samaki 9 na timba 04 zilizotelekezwa na wavuvi wasiojulikana  baada ya kupokea taarifa ya uwepo wa askari wanaofanya doria katika kisiwa hicho. Jeshi la polisi bado linaendelea na upelelezi pamoja na msako wa kuwasaka wavuvi wanaojihusisha na uvuvi haramu ili waweze kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Baada ya zana hizo haramu kukamatwa ziliteketezwa kwa moto mbele ya uongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya na serikali ya vijiji hivyo na wananchi wakishuhudia, huku msako na doria katika visiwa hivyo na visiwa vingine vya jirani bado unaendelea.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa wananchi akiwataka waendelee kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwani limedhamiria kukomesha uhalifu katika mkoa wa Mwanza na kusimamia sheria na taratibu za nchi.
Katika tukio la pili
Mnamo tarehe 08.06.Majira ya saa 13:06 katika kijiji cha Sima kata ya Sima wilaya ya Sengerma mkoa wa Mwanza, askari wakiwa doria walifanikiwa kumkamata Sophia Sato miaka 54 mkazi wa kijiji cha Sima akiwa na pombe aina ya gongo lita 64 zikiwa ndani ya nyumba yake kitendo ambacho ni kinyume na sheria na taratibu za nchi.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa anafanya biashara hiyo ya kuwauzia wananchi wa kijiji hicho pombe hiyo haramu na kuifanya kazi hiyo kama  chanzo chake cha mapato kitendo ambacho ni uvunjwaji wa sheria, ndipo jeshi la polisi lilipokea taarifa kutoka kwa raia wema na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa pindi uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Aidha katika tukio lingine sawa na tarehe tajwa hapo juu majira ya saa 13:50 katika kijiji hicho cha Sima kilichopo wilaya ya Sengerema, askari waliokuwa doria walifanikiwa kukamata mitambo miwili ya kutengeneza pombe  haramu ya gongo na mapipa mawili yaliyotelekezwa na Elizabeth Martine aliyetoroka baada ya kupewa taarifa za uwepo wa askari wanaofanya doria.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa tajwa hapo juu amekuwa akijihusisha  na utengenezaji wa pombe hiyo haramu kwa muda sasa, na amekuwa akiwauzia wakazi wa kijiji hicho. Jeshi la polisi linaendelea na msako wa kumtafuta mtuhumiwa pamoja na kuwasaka wahusika wengine anaoshirikiana nao katika biashara hiyo haramu ya pombe ya gongo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa wananchi akiwaomba waendelee kushirikiana na jeshi la polisi ili tujenge sote kwa pamoja Mwanza salama zaidi na kuweza kukomesha uhalifu katika mkoa wetu.
Imesainiwa na:
Sacp: Ahmed Msangi
Kamanda wa Polisi (M) Mwanza
Leave A Reply