MWILI wa aliyekuwa mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya Deutsche Welle (DW) nchini Ujerumani, Isaac Muyenjwa Gamba umeagwa katika ibada ya kuaga mwili huo iliyofanyika leo Jumatano, Oktoba 31, 2018 nyumbani kwao, Bunda mkoani Mara.
Mwili wa Gamba ambao uliwasili nyumbani kwao jana nyumbani kwao Bunda kwa ajili ya amzishi ukitokea Dar es Salaam kupitia Mwanza.
Mazishi ya Gamba yanatarajiwa kufanyika leo kwenye makaburi ya familia yao yaliyopo nje kidogo ya Mji wa Bunda.
Viongozi mbalimbali wa vyama na siasa wakiwemo Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili ambaye amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, Katibu Mkuu wa Chadema -Zanzibar, Salum Mwalimu na wengine wamejitokeza na kuungana na wanafamilia pamoja na waombolezaji wengine kuaga mwili wa marehemu.
Gamba alikutwa akiwa amefariki chumbani kwake Alhamisi, Oktoba 18, mwaka huu, jijini Bonn nchini Ujerumani alikokuwa akifanya kazi zake.
Baada ya uchunguzi wa hospitali nchini Ujerumani, imegundulika kuwa kilichosababisha kifo chake ni kuvuja kwa damu kwenye ubongo (Brain Hemorrhage) yaani presha ya damu.
Akitoa salam za pole Bupilipili ameushukuru uongozi wote wa DW kwa kufanikisha shughuli zote za kuuleta mwili wa marehemu hadi kufika mjini Bunda na watu wote waliohakikisha mwili huo unafika salaama na kuwafariji familia.
PICHA NA DENIS MTIMA
Comments are closed.