Ibra Kadabra atia dole gumba Man U
MCHEZAJI wa kimataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic ‘Ibra Kadabra’ mwenye umri wa miaka 34 amejiunga rasmi na klabu ya Manchester United ya Uingereza huku akitamba kuandika kumbukumbu mpya katika historia ya ligi ya England. Ibrahimovic atakuwa akilipwa mshahara wa zaidi ya pauni £200,000 kwa wiki.
Mchezaji huyo aliyekuwa akicheza na klabu ya PSG ya Ufaransa amesaini mkataba wa mwaka mmoja na tayari kocha wake Jose Mourinho amesema kuwa haihitaji kutoa sababu nyingi kuelezea kwa nini ameamua kumsajili mshambuliaji huyo kwa vile ‘takwimu zinajieleza’.
Wawili hao walikutana kwa mara ya kwanza wakati walipokuwa katika klabu ya Inter Milan ya Italia na kwamba sasa wanakutana tena wakiwa nchini Uingereza.
Ibrahimovic akisaini mkataba wa mwaka mmoja kuiceheza Klabu ya Man U
Ibrahimovic ambaye amekuwa akisifika kwa kupachika mabao ya kushtukiza ameandika kwenye mtandao wake wa Twitter akisema kuwa ‘”ninayo furaha kubwa kujiunga na klabu hii lakini jambo kubwa kwangu ni kufanya kazi tena kocha Jose”
Rekodi ya Ibrahimovic chini ya Mourinho
League appearances – 35
League goals – 25
Cup appearances – 3
Cup appearances – 3
European appearances – 8
European goals – 1
Rekodi Kamili ya Ibrahimovic
Date of birth: October 3, 1981 (aged 34)
1999-01 Malmo – Games 47 Goals 18
2001-04 Ajax – Games 110 Goals 48
2004-06 Juventus – Games 92 Goals 26
2006-09 Inter Milan – Games 117 Goals 66
2009-10 Barcelona – Games 46 Goals 22
2010-12 AC Milan – Games 85 Goals 56
2012-16 PSG – Games 180 Goals 156
2001-16 Sweden – Games 116 Goals 62
TOTAL: Games 793 Goals 454
Honours: Eredivisie (2002, 2004), KNVB Cup (2002), Serie A (2007, 2008, 2009, 2011), Italian Super Cup (2006, 2008, 2011), La Liga (2010), Spanish Super Cup (2009, 2010), UEFA Super Cup (2009), FIFA World Club Cup (2009), Ligue 1 (2013, 2014, 2015, 2016), Coupe de France (2015, 2016), Coupe de la Ligue (2014, 2015, 2016), Trophee des Champions (2013, 2014, 2015)