Ini Edo afungua bonge la ukumbi!
Mimz Lounge ya In Edo
MREMBO asiyechuja kunako filamu Nollywood, Ini Edo amezidi kujiongezea utajiri baada ya juzikati kufungua bonge la klabu na kulipa jina la Mimz Lounge.
Staa wa filamu za Nollywood, Ini Edo
Staa huyo alizindua mjengo wake huo pande za Lekki, Lagos, Jumatatu iliyopita na umeshaanza kutumika rasmi kuanzia juzi Jumatano. Mbali na klabu hiyo, pia kuna sehemu ya nyumba za kulala wageni ‘gesti’.