Jay Moe: Msiba wa Ngwair Sikulia Kama wa Langa
MKONGWE asiyechuja kwenye muziki wa Hip Hop Bongo, Juma Mchopanga ‘Jay Moe’ amefunguka kuwa alipofariki msanii mwenzake Ngwair alijikaza na akafanikiwa kutolia lakini alipofariki Langa, alimwaga machozi.
Akipiga stori na Showbiz Extra, Jay Moe alisema ingawa Ngwair alikuwa ni mshkaji wake wa karibu lakini siku ya msiba wake, alijikaza ila alipofariki Langa alishindwa kujizuia kutokana na msanii huyo kufariki siku chache baada ya kumueleza kuwa ameacha madawa ya kulevya.
“Nilikuwa na mvutano na marehemu Langa kwa muda mrefu kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya, siku chache kabla ya kifo chake alinieleza kuwa yupo poa na ameacha unga.
“Alinitaka tufanye kazi ya pamoja, hata hivyo tukiwa hatujakamilisha mpango huo nikapokea tarifa za kifo chake, kwa kweli nilumia sana,” alisema Jay.
NA ALLY KATALAMBULA | GAZETI LA AMANI