Jose Mara atikisa na New Mapacha Watatu
Stori: Uwazi Showbiz
WAPENZI wa Muziki wa Dansi nchini, hivi karibuni walimshuhudia Mwanamuziki Jose Mara akitumbuiza peke yake kwenye tamasha la muziki huo kufuatia kukimbiwa na Khalid Chokoraa na Kalala Junior waliyekuwa wanaunda Kundi la Mapacha Watatu.
Katika tamasha hilo lililojulikana kwa jina la Tanzania Band Festival lililozikutanisha bendi nyingi kwa ajili ya kumsapoti Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda katika kampeni ya kuchangia madawati.
Jose Mara alipanda jukwaani akiwa pamoja na wapiga vyombo pekee jambo lililofanya apigiwe shangwe za kutosha pia alisema bendi yake sasa inajulikana kwa jina la New Mapacha Watatu.