Jose Mara, Kalala Jr Kurejesha Mapacha wanne leo
Msanii wa muziki wa Dansi Bongo, Joseph Michael ‘Jose Mara’.
Wasanii wa muziki wa Dansi Bongo, Joseph Michael ‘Jose Mara’, na Charles Gabriel ‘Chaz Baba’, Jumamosi hii (leo) wanatarajia kuirejesha bendi yao ya Mapacha Wanne, ambayo ilikuwa ikiundwa na mastaa wenzao wawili Khaleed Chuma ‘Chokoraa’ na Junior Kalala ‘Kalala Junior.’
Mapacha Watatu (Jose Mara, Khalid Chokoraa na Kalala Junior).
Wasanii hao usiku wa leo watafanya makamuzi ya pamoja ndani ya Ukumbi wa Mango Garden Kinondoni jijini Dar es Salaam, ikiwa ni moja ya mwendelezo wa kundi hilo ambalo lilisamb- aratika baada ya Chaz Baba kuzuiwa na bendi yake ya zamani ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, huku Kalala Junior naye akijiengua kwenye bendi hiyo na kuwaacha Jose Mara na Chokoraa.
Akizungumza na gazeti hili Jose Mara alisema leo watawakumbusha mashabiki zao namna walivyokuwa wakifanya wakati wapo kwenye kundi moja, mbali na hivyo pia itakuwa ni mwanzo wa kujenga umoja wa Mapacha Wanne, kwani wanatarajia kupiga shoo zaidi ya moja nje ya Jiji la Dar.
“Kweli leo Mapacha Wanne itarudi kwani tutafanya makamuzi ya nguvu hivyo nawaomba watu waje kutushuhudia kwani tutakuwa tukitoa burudani na kujenga umoja wa Mapacha Wanne, tutasindikizwa na Twanga Pepeta,” alisema Jose Mara.
Comments are closed.