RAIS John Magufuli, leo Jumatano, Oktoba 9, 2019, ameanza ziara ya siku tatu mkoani Katavi ambapo amefungua barabara ya Kanazi – Kizi – Kibaoni yenye urefu wa Kilomita 76.6.
Magufuli yupo katika ziara ya siku tisa katika mikoa ya Songwe, Rukwa na Katavia ambapo amewasili katika Uwanja wa Kibaoni wilayani Mlele mkoani Katavi na kuzungumza na wananchi wa eneo hilo akiwa ameambatana na mkewe, Janeth Magufuli, na mawaziri mbalimbali.
Akizungumza na wananchi, amewahakikishia wananchi wa Katavi kuwa miradi mingi mkoani humo itatekelezwa kwani fedha zipo.
“Hela zipo. Mafisadi wameanza kurudisha hela, kwa nini tuache kujenga hapa?” amesema.
Pia ameagiza kuanzishwa kwa chuo cha utafiti wa kilimo mkoani humo na kusema vijiji 920 yakiwemo mapori tengefu 12 na misitu ya hifadhi ifutwe, ikiwemo kumega hifadhi ili kusaidia wananchi kuendeleza kilimo wakati vijiji 60 vilivyokuwa na migogoro ya ardhi vikiachiwa na kuwa vijiji rasmi.
MSIKIE RAIS MAGUFULI
Comments are closed.