Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Hamis Juma leo Julai 4 mwaka huu ametembelea Maonyesho ya sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Akiwa viwanjani hapo mbali na kutembelea mabanda mengine pia ametembelea banda la Mahakama Kuu ya Tanzania na kujionea shughuli mbalimbali zikiendelea za mahaka hiyo vitengo mbalimbali ambapo mara ya kumaliza alisema kwa sasa wanajitahidi kumaliza kesi zote zilizopo katika mahaka katika kipindi cha miezi tisa ili ziwe zinapungua.
PICHA NA DENIS MTIMA| GLOBALPUBLISHERS