The House of Favourite Newspapers

Katika Kuhitimisha Krismasi, Shigongo Asherehekea Na Wakazi Wa Pupandwa

0
Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja akiendesha misa fupi  Bupandwa Mhela ya kuwakumbuka wazazi wa Eric Shigongo na ndugu wengine walio mbele za haki.
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo akishiriki ibada fupi ya kuwakumbuka wapendwa wake waliotangulia mbele za haki, akiwemo baba yake mzazi, James Bukumbi na mama yake Bi. Asteria Kapela  na kusherehekea sikukuu ya Krismasi  katika Kijiji Cha Bupandwa Mhela, Wilaya ya Sengerema Mwanza.
Kushoto ni Mjukuu wa Marehemu, James Bukumbi aitwaye James akishiriki ibada fupi kijijini Bupandwa Mhela.
Kwaya ya Mt. Maria Parokia ya Bupandwa akiwa imeketi baada ya kumaliza kuimba nyimbo zao.
Diwani wa Kata ya Bupandwa Mhela, Masumbuko Francis (wa pili mbele kushoto) akishiriki ibada fupi nyumbani kwa Mkurugenzi wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo pamoja na wananchi wengine.
Mkurugenzi wa Global Publishers, Lydia James Bukumbi (wa kwanza kushoto) akishiriki ibada fupi.

Wakati sikuku ya Krismasi ikiwa imemalizika jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo amesherehekea sikukuu hiyo kwa kufanya Misa fupi ya kuwakumbuka wapendwa wake waliotangalia mbele za haki akiwemo baba yake mzazi Marehemu, James Bukumbi na Bi. Asteria Kapela ambao wote wapo mbele za haki.

 

Akiendesha ibada fupi Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja amewataka wakazi wa Bupandwa na vitongoji vingine vilivyoungana katika misa hiyo kutenda matendo mema yenye kuumpendeza mungu katika kipindi hiki cha kusherehekea sikukuu ya Krismasi na Mwaka mpya.

 

Amesema kuwa mwanadamu anapaswa kufanya yale yote yanayompendeza Mungu,kuoneshaa upendo kwa ndugu jamaa na marafiki hata kama upo katika ngazi mbalimbali za kiserikali ama kidhehebu kuonesha umoja na mshikamano ili hata ukifa matendo yako yampendeze mungu.

 

Kwa upande wa familia, Bi Leah Bukumbi amewataka wakazi wa Bupandwa kushikamana kattika shida na raha, kuimarisha upenndo ili kutokusababisha mgawanyiko. Amesema kuwa familia ya Bukumbi inawapenda sana wakazi wa Bupandwa na itahakikisha inashiriki katika shughuli zote za kijamii na kifamilia ili kuendeleza umoja waliouacha wazazi wao ambao siku ya leo wanaukumbuka kwa kuwaombea.

Leave A Reply