Kichupa kipya cha Man Fongo Shilole ageuka video queen
Amani Fongo ‘Man Fongo’
MAYASA MARIWATA
MSANII wa Muziki wa Singeli, Amani Fongo ‘Man Fongo’ anatarajia kuachia video ya ngoma yake ya Hainaga Ushemeji huku mwanadada, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ akijiachia kama video queen.
Akipiga stori na Showbiz Xtra Man Fongo anayebamba na Ngoma ya Hauna alisema kuwa, ameamua kutoa video ya ngoma hiyo kwa kuwa imepokelewa vema na mashabiki.
Amani Fongo ‘Man fongo’ na Zuwena Mohammed ‘Shilole’
“Wiki ijayo natarajia kuachia Video ya Hainaga Ushemeji. Ninavyofanya huu muziki siyo kama walivyo wasanii wanaoimba Singeli na ngoma za uswazi, naenda na wakati na ndiyo maana nikamchukua Shilole kama video queen ili kuinogesha zaidi,” alisema Man Fongo.