KESI namba 457 ya Jamhuri dhidi ya JamiiForums (inayohusu Kampuni za CUSNA Investment & Ocean Link kudaiwa kukwepa kodi katika Bandari ya Dar es Salaam, kuchonga nyaraka kutorosha makontena na kunyanyasa wafanyakazi wa kitanzania) imeahirishwa hadi Februari 15, 2018 kutokana na kukosekana kwa shahidi wa upande wa Jamhuri mahakamani hapo.
Watuhumiwa wanadaiwa kushindwa kutoa taarifa kuhusu mmiliki wa akaunti moja iliyosajiliwa JamiiForums huku wakijua kwamba jeshi hilo linafanya uchunguzi wa makosa ya jinai yaliyochapishwa kielektroniki kwenye tovuti hiyo.
Mpaka sasa mashahidi 5 wa Jamhuri wameshasikilizwa katika kesi hiyo ambayo imepigwa kalenda hadi Februari 15, 2018 kwa ajili ya kusikilizwa.
Comments are closed.