The House of Favourite Newspapers

KMKM Wafungashiwa Virago Kagame Cup

0

WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya Kagame Cup 2021, KMKM safari imewakuta kwa kushindwa kutinga hatua ya fainali. Katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Azam Complex, Agosti 10 baada ya dakikq 90 ubao ulisoma Express 2-1 KMKM.

 

Bao la mapema la Ibrahim alilopachika dk 45 halikuweza kuwapa ushindi KMKM kwani lilidumu kwa muda wa dk 11. Dakika ya 56 Muzamiru Mutyaba aliweka usawa bao hilo na bao la ushindi lilifungwa dk 90+4 na Kambale kwa mkwaju wa penalti. Sasa fainali itakuwa kati ya Express v mshindi wa mchezo wa leo kati ya Azam FC v Nyassa Big Bullets.

Leave A Reply