The House of Favourite Newspapers

Waziri Mkuu, Majaliwa Aahirisha Bunge Hadi Novemba

0
Waziri Mkuu, Kasimu Majaliwa.

WAZIRI Mkuu, Kasimu Majaliwa akitoa Hoja ya Kuahirisha Bunge mjini Dodoma leo amefafanua kuhusu hali ya wakulima na changamoto wanazokumbana huku akielezea mikakati ya Serikali ya Awamu ya Tano inavyopambana na changamoto kwa lengo la kukuza kipato cha mkulima.

Majaliwa amelieleza Bunge kuwa serikali imechukua jitihada za dhati za kuwataftia masoko wakulima pamoja na kupunguza tozo la kodi mbalimbali kwenye mazao.

Akizungumzia masuala ya elimu, Waziri Mkuu amewasihi wazazi na wananchi kuendelea kutoa ushirikiano ili kukuza sekta hiyo. Ambapo Sekta Afya na Hatua ya Kimaendeleo iliyopiga katika sekta hiyo na jinsi wanavyo kabiliana na changamoto zote wanazo kumbana nazo.

Majaliwa pia ameeleza kuwa serikali inafanya jitihada kubwa kuwezesha sekta ya vijana na hususani kuwasadia katika kupata ajira.

Baada ya kutoa maelezo hayo, Majaliwa aliwashukuru wabunge wote wa bunge hilo tukufu na kutoa hoja ya kuahilisha Mkutano wa Nane wa Bunge hadi Novemba 7, 2017.

Leave A Reply