The House of Favourite Newspapers

LIVE Kutoka Bungeni, Uwasilishwaji wa Bajeti Kuu ya Serikali 2017/2018

0
Serikali imetoa takwimu ikielezea hali ya ukuaji uchumi katika kipindi cha mwaka 2016 na kueleza kuwa kiwango hicho kimeendelea kukua kwa wastani wa asilimia saba ikiwa ni pungufu kidogo ya kile kilichotarajiwa awali.
Akisoma hotuba ya mwelekeo wa hali ya uchumi wa Taifa bungeni leo Alhamisi,  Waziri wa Fedha na Mpango , Dk Philip Mpango amesema makadirio ya awali yalionyesha kuwa uchumi huo ungekua kwa wastani wa asilimia 7.2.
“ Hali ya ukuaji uchumi imeendelea kushuhudiwa katika kiwango  kilekile cha awali cha asilimia saba na hii imechangiwa na mambo mengi ikiwamo  baadhi ya sekta kutofanya vizuri,” amesema.
Ametaja baadhi ya sababu hizo kuwa ni pamoja na kushuka wa sekta ya kilimo iliyotarajiwa kukua kwa asilimia 2.9, lakini malengo hayo hayakufikiwa na badala yake yalikuwa kwa asilimia 2.1.
Pia, amegusia sekta ya biashara aliyosema ilikuwa kwa asilimia 6.7 hali ambayo ni tofauti na makadirio yaliyowekwa awali yaliyokuwa asilimia 7.8.
Eneo la chakula nalo limetajwa kuchangia kushindwa kufikia kwa malengo ya ukuaji wa uchumi.
“Makadirio yetu yalikuwa kwamba sekta ya chakula ingekua kwa asilimia nane, lakini bahati mbaya ilishuka na kuwa asilimia 3.7,”amesema.
Hata hivyo, alikumbusha namna sekta nyingine zilivyoweza kufanya vizuri na kusaidia uchumi wa Taifa kuendelea kuhifadhi kiwango chake. Baadhi ya sekta hizo ni pamoja na habari na mawasiliano, madini na kiashirio cha kuendelea kukua kwa sekta ya viwanda.

Leave A Reply