JUMUIYA YA WAZAZI CCM YAAHIDI KUMTETEA MAGUFULI
Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, imeahidi kuendelea kumtetea Rais Magufuli dhidi ya watu wanaombeza na kudharau kazi kubwa ya kuiletea maendeleo nchi anayoifanya.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Rodrick Mpogoro, katika Mkutano wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere, Posta jijini Dar es Salaam.
Katika hotuba yake, Mpogoro amewataka wanajumuiya hiyo kuwa wamoja na imara katika kutekeleza azma ya chama hicho kuendelea kukua katika mashina mbalimbali ya serikali za mitaa.
Comments are closed.