JPM: Uwaziri Mkuu Hauna ‘Guarantee’, Nampa Pole Majaliwa… – Video
RAIS John Magufuli amesema kuwa kazi ya Uwaziri Mkuu haina dhamana kwamba kila atakayeteuliwa atakaa kwa miaka mitano kwani anaweza kufanya mabadiliko wakati wowote kulingana na utendaji wa mtu husika aliyepo kwenye wadhifa huo.
Amesema hayo leo Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, leo Jumatatu, Novemba 16, 2020, wakati akimwapisha Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, na kuongeza kuwa kuendelea kwake kukaa madarakani kutategemea na utendaji wake kwa kipindi cha pili cha serikali ya awamu ya tano,
“Nawapongeza walioapa leo, Mawaziri wawili na Waziri Mkuu, sikuwa na haraka sana ya kuteua Baraza la Mawaziri, tuna Wabunge zaidi ya 350, na bado kuna nafasi 10 za mimi kuteua, wabunge presha mzishushe, kazi mliyoomba ni ubunge sio uwaziri.
FUATILIA TUKIO ZIMA HAPA