JPM Atoa Siku 60 Kwa Mashirika na Taasisi Yasiyotoa Gawio – Video
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo Novemba 24, 2019 amepokea gawio, michango na ziada ya Serikali kutoka mashirika, kampuni na taasisi mbalimbali ambazo zinamilikiwa na Serikali.
Hafla ya kupokea gawio, michango na ziada hiyo inafanyika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Akiongea katika hafla hiyo amesema haya ”Tuna mashirika na taasisi mbalimbali 266 mpaka leo ambayo yamechangia gawio kwa Serikali ni 79, nawapongeza sana mliochangia zaidi ya Tilioni 1 kwa ajili ya manufaa ya taifa hili.
”Yapo mashirika ambayo mishahara yao inalipwa na Serikali wamepewa nyumba wengine sasa ndugu zangu mnaweza kujiuliza ungekuwa wewe ndo Rais ungefanyaje tena unaweza kukuta wengine wamelala kwenye hoteli wanatuangalia kwenye TV” ameyasema Rais Magufuli
Comments are closed.