The House of Favourite Newspapers

JPM Ataja Sababu za Kumchagua Majaliwa – Video

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli leo Jumatatu, Oktoba 15, 2019 amezungumza na Wananchi wa Jimbo la Ruangwa.

 

“Kufanya kazi na mimi ni kazi ngumu, lazima ujipange sawa sawa na hili nawaeleza ukweli sababu na mimi ni mgumu, lakini ndugu Kassim Majaliwa ameweza, nilihitaji mtu ambaye atanisaidia kutumbua hata kwa kushika mikasi.

 

“Waziri Mkuu naona mpole huku jimboni eeeh? Usiniache mimi nije kutoka Dar nije nitumbue hapa wakati mkasi na visu vya kutumbulia vyote nilikukabidhi wewe.

 

“Waziri Mkuu Hongera sana unanisaidia sana kazi, wengine wanaweza sema nakupa kichwa ila ukweli ni huo na una kichwa kizuri,unafanya napumzika nikikutuma sehemu unafanya kazi Kwahiyo wanaochonga wachonge sana wanaonuna wanune ila sikutoi utaendelea kuwa Waziri Mkuu.

 

“Mhe. Majaliwa ananisaidia sana, akishirikiana na Wabunge wa Mkoa huu wa Lindi na wako hapa , Mbunge Mama Salma Kikwete, Wabunge wengine wapo wapi? Mhe. Nape, sogea hapa Nape karibu na Mama Salma,” amesema Rais Magufuli.

 

Comments are closed.