JPM na Museveni Wasaini Mkataba Ujenzi Mradi wa Bomba la Mafuta -Video
Rais John Magufuli wa Tanzania na Rais Yoweri Museveni wa Uganda leo Septemba 13, 2020 wamesaini makubaliano ya kuanza ujenzi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga
Rais Magufuli amesema hatua hiyo ni ya muhimu sana kuelekea utekelezaji wa mradi huo wenye thamani ya takriban Dola za Marekani Bilioni 3.5
Ameongeza kuwa, hapa nchini bomba litapita kwenye Mikoa 8, Wilaya 24 na Kata 132. Aidha, watu zaidi ya 90,000 watalipwa fidia inayokadiriwa kufikia Bilioni 21
Rais Magufuli amempongeza Rais Museveni akisema amefanya mambo yasiyowezekana na endapo mafuta hayo yasingepatikana Uganda, Tanzania isingenufaika