The House of Favourite Newspapers

Liverpool Yatwaa Ubingwa Carabao Cup 2022

0

Liverpool imetawazwa kuwa mabingwa wapya wa Kombe la ligi (Carabao Cup) msimu huu, baada ya usiku wa kuamkia leo kuitandika Chelsea kwa mikwaju ya penati 11-10 katika uwanja wa Wembley.

Mpaka dakika 120, timu hizo zilienda sare ya bila kufungana. Mlinda mlango wa Chelsea anayetajwa kama mtaalamu wa kuokoa penati Kepa Arrizabalaga, aliingizwa katika dakika za mwisho kwa ajili ya kuisaidia timu yake, alikosa penati muhimu baada ya mwenzake wa Liverpool Caoimhin Kelleher, kufunga mkwaju wake.

Wachezaji wote wa Liverpool walipata penatiki akiwemo Kipa Kelleher aliyefunga penati ya mwisho ya 11 lakini Kepa alipaisha juu penati yake, na kuhitimisha mchezo kwa machungu.

Katika mchezo huo, magoli 3 ya Chelsea yalikataliwa ikionekana wachezaji wamezidi (offside). Kiungo wake Mason Mount atakuwa na usingizi wa mang’amung’amu wiki hii baada ya kukosa nafasi mbili muhimu za kufunga, huku mlinda mlango wake Edouard Mendy, akiokoa michomo mengi ya Liverpool.

Liverpool wao walitengeneza nafasi nyingi katika mchezo huo, huku goli la Joel Matip likikataliwa kutokana na madhambo yaliyofanyika na kuotea kabla ya kufunga.

Ni kombe la kwanza kwa Liverpool msimu huu, likiweka rekodi kwa timu hiyo kulitwaa mara 9, wakiendelea kuwania pia makombe mengine ya ligi kuu, mabingwa Ulaya na FA Cup.

Leave A Reply