The House of Favourite Newspapers

Lugola Awasimamisha Kazi OCD, OCS na OC CID, Kisa Mahabusu 15 Kutoroka

 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amewasimamisha kazi Mkuu wa Polisi Wilaya ya Geita (OCD), Mkuu wa Kituo cha Polisi Geita (OCS) na Mkuu wa Upelelezi Wilaya hiyo (OC CID), kwa kosa la Mahabusu kutoroka Mahakamani. Na pia ameelekeza Askari 8 wa kituo hicho wawekwe Selo.

 

Mei 21, 2019 mahabusu 15 wanadaiwa kutoroka wakati wakisubiri kuitwa kwa ajili ya kesi zao. Imeelezwa kuwa mahabusu hao walifungua mlango wa nyuma wakati askari wakiwa nje ya lango kuu la kuingia katika ukumbi walikokuwa wamewekwa. Hadi sasa mahabusu wanne wameshakamatwa.

 

BREAKING: LUGOLA ‘Awasweka’ Ndani ASKARI Wake, Wengine AWATUMBUA, Kisa Hiki…!!

Comments are closed.