Lukaku Akutana na Jay-Z, DJ Khaled Nchini Marekani
ROMELU LUKAKU anayelipiga soka na timu ya Manchester United ya Uingereza, ametimiza ndoto yake kwa kukutana na rapa Jay-Z na prodyuza DJ Khaled, wote wa Marekani.
Alikutana na mastaa hao huko New Jersey hivi karibuni wakati wa ziara ya muziki ya Jay-Z na mkewe, Beyonce, iitwayo ‘On the Run II Tour’ wakati wakitumbuiza katika dimba la MetLife Stadium huko East Rutherford, New Jersey.
Lukaku alikuwa katika mapumziko baada ya timu yake kutoka katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi iliposhika nafasi ya tatu.
Comments are closed.