The House of Favourite Newspapers

Lulu bado hajiwezi kwa Bieber

0

lulu mungu (3)STAA wa filamu Bongo, Elizabeth Michael amesema kuwa bado anateswa na penzi la staa wa muziki wa Pop, Justin Bieber na kwamba yupo tayari hata kuchukuliwa bure.

bieber

Chanzo makini kiliitonya Amani kuwa, staa huyo uvumilivu umemshinda kila aonapo sura ya Bieber popote na hata majuzi alimng’ang’ania sana staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akionana naye amfikishie ujumbe kuwa anampenda.

“Imekuwa kero sasa, hivi karibuni alimtumia ujumbe Diamond kuwa akienda kwenye sherehe za upokeaji wa Tuzo za MTV EMA asisahau kumfikishia ujumbe Bieber kuwa hajiwezi kwake,” kilisema chanzo.

Lulu alipovutiwa waya juu ya kumpenda kwake Bieber alikiri kumpenda.

Leave A Reply