MGOMBEA urais Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif, amefika katika kituo cha Garagara, Jimbo la Mwera, na kupiga kura mapema leo Jumatano, Oktoba 28, 2020.
Aidha, amesema ametiwa moyo na watu wengi kujitokeza katika vituo vya kupigia kura ila amegundua wananchi wengi wana malalamiko ya kutokuona majina yao kwenye vituo walivyojiandikisha.