Magufuli ahahidi neema kwa wavuvi, wachimbaji wadogowadogo Mwanza na Geita
Dk John Magufuli akihutubia nyomi la watu lililofurika katika Kijiji cha Nkome, Geita Vijijini.
Baada ya kuzuru makaburi hayo kwenye Kijiji cha Katoma kilichopo Geita Vijijini, Magufuli aliingia kwenye nyumba hii ya babu yake na kuwajulia hali ndugu zake.Bibi huyu alinaswa na kamera yetu akimsikiliza Magufuli kwa hisia kali wakati akiwahutubia wakazi wa Nkone, Geita Vijijini.Msanii wa Bongo fleva, Linnah Sanga akikamua kwenye jukwaa la mkutano Kijiji cha Nkome, Geita vijijini leo
Magufuli akiwahutubia wakazi wa Kamanga jimbo la Sengerema.Magufuli akiendelea kumwaga sera kwa wakazi wa Nkome, Geita VijijiniMagufuli akizungumza na wakazi wa Kalebezo jimbo la Sengerema.Magufuli alivyoomba kura kwa wakazi wa Buchosa kwenye mkutano uliofanyika katika Mji mdogo wa Nyehunge, Sengerema, Mwanza.
Malaika akifanya yake jukwaani.Msafara wa Magufuli ukitoka Mwanza kuelekea Sengerema kupitia Kamanga kwa kivuko cha Mv Samar. Mwanadada Rubby naye akifanya yake jukwaani. Chege na Temba nao kama kawa. Vimbwanga vya Ze Orijino Komedi, kijiji cha Nkome.Wakazi wa Bugulula wakimsikiliza Magufuli wakati wakiwa juu ya paa.Wakazi wa Geita Vijijini wakionesha furaha ya kumkubali Magufuli.Wakazi wa Jimbo la Buchosa wakiinua mikono kuonesha kumkubali Magufuli kwenye mkuatno uliofanyika Nyehunge.
Katika mikutano hiyo Magufuli aliwaahidi wakazi hao kuwaboreshea miundombinu ya uvuvi katika Ziwa Victoria kwa kuwapatia wavuvi wadogo mikopo na kuwaletea vitendea kazi bora.
Akiwazungumzia wachimbaji wadogo wa madini nao aliwaahidi kuwaboreshea kazi yao.
Magufuli aliwaahidi wakazi hao kuwaongea huduma ya zahanati bora zitakazotoa huduma bila ubabaishaji na kuwaboreshea barabara za maeneo hayo kwa kiwango cha lami ili kuzipa soko biashara zitakazokuwa zikifanyika ukanda huo.