Mahakimu 11 Wafukuzwa Kazi, Wengine 30 Kikaangoni
Katika hatua nyingine, Mahakama Maalumu ya Ufisadi na Uhujumu Uchumi imeanza rasmi na wiki ijayo Kanuni za Uendeshaji wa mahakama hiyo, zinatarajiwa kuchapishwa.
Awali akiwasilisha taarifa za utendaji wa Mahakama Kuu, Mahakama za Hakimu Mkazi, Wilaya na za Mwanzo, Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugeta alisema baada ya uchaguzi, walipokea kesi 247 za uchaguzi, 53 za kupinga matokeo ya ubunge na 194 za udiwani.
Kwa upande wake, Msajili wa Mahakama ya Rufaa, John Kahyoza alisema kiwango cha kumaliza mashauri katika Mahakama ya Rufaa kimeongezeka, pia wana lengo la kuhakikisha nakala za hukumu zinapatikana siku hukumu na ndani ya siku tatu zitapatikana kwenye tovuti ya Mahakama ya Tanzania.
Katika hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya Sheria Februari 4, mwaka huu, Rais Magufuli alisema anaitegemea sana Mahakama na aliwaambia majaji na mahakimu nchini kuwa:
I love this president