The House of Favourite Newspapers

MAIMATHA NA MASHOSTI WA WEMA

MTANGAZAJI Maimartha Jesse ‘Mai’ amesema anaukubali msimamo wa muigizaji Wema Sepetu wa kukaa mbali na marafiki alioutangaza hivi karibuni kwani utamweka sehemu nzuri.

Akipiga stori na Za Motomoto, Mai alisema kuamua hivyo ni jambo zuri kwa sababu sio lazima kuwa na marafiki ila kinachotakiwa ni kuwa mstarabu na watu wanaomzunguka.

 

“Mimi Wema ni dada yake sipo kwenye kundi la marafiki kwa hiyo ushirikiano wetu upo katika mambo mbalimbali ya maendeleo na kwangu anaweza kuja muda wowote hata kwa ushauri,” alisema Mai.

Mai aliongeza kuwa, hatua aliyofikia Wema kwa sasa ni kutulia na kuangalia maisha yanavyoenda kwani Wema bado umri unamruhusu na anatakiwa kutulia.

ZAINA MALOGO

Comments are closed.