The House of Favourite Newspapers

Mainda: Mitandao Imeharibu Msiba wa Patrick

MKONGWE kwenye Tasnia ya Filamu Bongo, Ruth Suka ‘Mainda’ amefunguka kwa uchungu kuwa, kama sio timu za kwenye mitandao ya kijamii hususan Instagram, mtoto wa muigizaji Rose Alphonce ‘Muna’, Patrick angezikwa vizuri bila kutokea figisu zilizotokea.

Akizungumza hivi karibuni akiwa msibani Mwananyamala-Kisiwani jijini Dar, Mainda alisema anaamini watu wa mitandaoni wamechangia kwa kiasi kikubwa kuweka taarifa za upotoshaji kati ya Muna na mumewe Peter ambazo zimesababisha wawili hao washindwe kuelewana haraka.

“Jamani hivi ni vitu gani? Ndiyo maana mimi sipo kwenye mitandao nina sababu kubwa sana. Kuna upotoshaji wa hali ya juu na kama isingekuwa mambo ya matimu haya kusingetokea mvutano mkubwa uliokuwepo na kusababisha mambo mazito kwenye msiba wa mtoto asiyekuwa na hatia kabisa,” alisema Mainda huku akilia.

Mwili wa Patrick ulipumzishwa katika makazi yake ya milele juzi Jumamosi kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar.

 

STORI: Imelda Mtema, DAR

Comments are closed.