MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI KAMALA HARRIS AHITIMISHA ZIARA YAKE TANZANIA-(VIDEO+PICHA)
MAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris leo Machi 31, 2023 amekamilisha ziara yake ya kikazi nchini Tanzania na kuelekea Zambia ambako atahitimisha ziara yake barani Afrika.
Akiwa Tanzania amekutana na mwenyeji wake, Rais wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, Ikulu Dar es Salaam na kuzungumza mambo mbalimbali ikiwepo kuimarisha ushirikiano wa mataifa haya mawili na masuala ya kiuchumi.
Pia, viongozi hao wamezungumza namna Tanzania inavyofanya vizuri kuimarisha demokrasia, na kuinua wanawake kiuchumi ambapo Kamala amempongeza Rais Samia kwa hatua mbalimbali alizochukua ikiwemo kuruhusu mikutano ya hadhara na kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari.
Kamala amekuwa na takribani wiki moja ya ziara ya kikazi barani Afrika ambapo ziara yake ilianzia Ghana.