The House of Favourite Newspapers

Mama Akutana na Mwanaye Aliyepotea Zaidi ya Mwaka Kupitia Video ya Wanandoto

kala-jeremiah-2

 Mama Adam akiwa na mwanaye jana kwenye kituo cha kulelea watoto cha CHAKUWAMA.

kala-jeremiah-3Kala Jeremiah akiwa katika pozi na Adam siku ya kuandaa video ya wimbo wa Wanandoto.

MAMA wa mtoto mmoja aitwaye Adam mwenye umri wa miaka 14, amefanikiwa kukutana na kijana wake huyo baada ya kupotezana naye kwa zaidi ya mwaka mmoja na hatimaye kumuona kwenye video ya wimbo wa mwanamuziki wa Hip Hop, Kala Jeremiah uitwao WANANDOTO.

Akiongea na tovuti hii, Kala anasema;

“Siku tatu zilizopita nilipigiwa simu na mtu mmoja akaniambia kuna mama kamuona mtoto wake kwenye video yangu ya Wanandoto na mtoto huyo alipotea tangu mwaka jana mwezi wa tisa, mama wa mtoto alifanya jitihada zote za kumpata mtoto wake bila
mafanikio.

“Juzi juzi mama huyo akiwa anatazama video ya WANANDOTO akamuona mwanaye huyo hali iliyopelekea kupata mshangao na mshituko ndipo alipoamua kumtafuta mtangazaji fulani wa redio ambapo mtangazaji huyo alinitafuta na kuniunganisha na mama huyo.”

Baada ya kukutana na mama Adam, Kala anasema mama alimueleza kwa masikitiko makubwa jinsi mtoto wake alivyopotea tangu Septemba mwaka jana na alimtafuta sana kila sehemu, kwa waganga wengi alienda, kwenye maombi ya kila aina lakini hakufanikiwa kumpata mwanaye mpaka alipokuja kumuona kwenye video ya Wanandoto.

Kala akiendelea kuchonga na tovuti hii, aliongeza;

“Baada ya mama huyo kunieleza yote hayo nikawasiliana na kituo cha kulelea watoto cha CHAKUWAMA ambapo mtoto Adam analelewa nikawaeleza habari hii wakakiri kweli Adam yupo na ni kweli walimpata mwaka jana mwezi wa tisa.

“Basi nikawasiliana tena na mama yake Adam na kumwambia kuwa nimewasiliana na mlezi wa kituo amekiri kuwepo kwa Adam kituoni hapo na kwakuwa mimi sipo Dar kwa muda huu nikamuunganisha mama Adam na mlezi wa kituo kile wakawasiliana na jana mama Adam amefika kituoni pale na kuonana na mwanaye na amefurahi sana.” Alimalizia staa huyo wa ngoma ya Wanandoto.

Video iliyopelekea mama Adam kumpata mwanaye hii hapa;

Comments are closed.