Mama Samia Awasili Serengeti Kuadhimisha Miaka 60 ya TANAPA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Seronera Wilaya ya Serengeti leo Disemba 22, 2019 kwa ajili ya kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 60 ya kuanzishwa kwa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya NGORONGORO (NCAA) yanayotarajiwa kufanyika kesho katika Hifadhi ya Ikoma Serengeti mkoani Mara.