Manyara: Ajali Yaua 6 Akiwemo Padri
Watu sita akiwemo padri wa kanisa katoliki parokia ya Masaktas jimbo la Mbulu mkoani Manyara, Sixtus Masawe wamefariki dunia katika ajali ya gari huko Monduli huku wengine sita wakijeruhiwa. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Salum Hamduni amethibitisha kutokea kwa ajali.