The House of Favourite Newspapers

Matunda Yanayosaidia Kupunguza Maumivu Ya Tumbo La Hedhi

 

 


MAKALA: UWAZI | AFYA

MZUNGUKO wa hedhi ni mzungu­ko wa kila mwezi am­bao mwanamke hu­upata, hali ambayo huleta kuto­kwa na damu kutokana na mimba kuto­tungwa.

Kwa hali ya kawaida hedhi ya kwanza hutokea katika umri wa miaka 12 -13 na kuendelea na hutokea pale ambapo tishu za ukuta wa mji wa mimba zinapobomoka na kutoka kama damu ukeni.

Tumbo la hedhi au mau­mivu wakati wa hedhi (pe­riod pains) au ki taalamu dismen­o r ­rhea, ni maumivu yanayo­jitokeza sehemu ya chini ya tumbo au kiunoni wakati mwanamke anapoanza kupata siku zake au kabla y a hapo.

Maumivu ya tumbo wakati wa hedhi huanza pale mayai yan­apotoka ka­tika mirija (fallopian tubes) na kuteremka chini ya mirija hiyo wakati wa Ovulation.


Maumivu ya tumbo la he­dhi yapo ya aina mbili. Aina ya kwanza au (Primary Dysmenorrhea) ni maumi­vu yasiyokuwa na sababu zozote za kimsingi za kitiba. Katika aina hii maumivu ni ya kawaida na huhisiwa se­hemu ya chini ya tumbo na kiunoni

Aina ya pili au (Second­ary Dysmenorrhea) ni yale maumivu yanayojumuisha maumivu yanayosababish­wa na sababu nyinginezo za kitiba kama vile mata­tizo katika kizazi, ugonjwa wa nyonga (PID) na mata­tizo katika mirija ya mayai.

Magonjwa pia husaba­bisha mwanamke kusikia maumivu ya tumbo la he­dhi. Miongoni mwa ma­gonjwa hayo ni endome­triosis. Hii ni hali ambayo seli za ndani ya mfuko wa uzazi huanza kuoka nje ya fuko hilo, au hata sehemu nyinginezo.

Leo ninayo orodha ya matunda ambayo yakitumika huweza kupunguza ma umivu wakati wa kipindi hi­cho.

Matunda hayo ni haya yafuatayo:-

 

NANASI

Hili ni miongoni kati ya matunda yenye uwezo wa kupunguza maumivu hayo yatokanayo na mzunguko wa hedhi, hii ni kutokana na tunda hili kuwa na viru­tubisho vyenye uwezo wa kuifanya misuli ya sehemu za siri za kike kuwa huru (kurelax) na hivyo kupun­guza uwezekano wa mau­mivu makali.

NDIZI

Kama utakuwa ni mfuatiliaji mzuri wa umuhimu wa matunda nadhani utakuwa umewahi kusikia kuhusu umuhimu wa ndizi hata kwa wanamichezo na im­ekuwa ikiwasaidia kureke­bisha misuli na kuondoa tatizo la kukaza kwa misuli mara baada ya mazoezi, hivyo basi tunda hili pia huweza kuwasaidia wa­nawake ambao wanapatwa na maumivu makali wakati wa hedhi na kupunguza au kuondoa hali hiyo kabisa.

Pamoja na kukueleza kuwa matunda hayo huweza kupun­guza maumivu wakati wa mzunguko la­kini ni vyema kuzingatia kuwa matunda hayo ya­napaswa kuliwa angalau siku mbili au moja kabla ya kuingia kwenye mzunguko wako ili kupata matokeo mazuri zaidi.

Pia unashauriwa kunywa tangawizi kila siku mara mbili, wiki moja kabla ya kupata mzunguko wako, pia maji ya kutosha kipindi cha mzunguko kwani nayo huwa na nafasi kubwa ya kusaidia kupunguza ki­wango cha maumivu hayo.

Papai bichi lililokomaa husaidia kupunguza mau­mivu ya hedhi unashau­riwa kulila mara kwa mara. Mboga za majani pia ni msaada mkubwa kwa ku­punguza maumivu.

Comments are closed.