The House of Favourite Newspapers

GF Trucks & Equipments Yaikabidhi Mbao FC Basi la Sh. Mil 70

0
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Nyamagana (CCM) Angelina Mabula akikata utepe kuzindua basi ambalo kampuni ya GF Truck & Equipments imelikabidhi kwa klabu ya Mbao FC ya Mwanza leo jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya mkataba wa miaka mitatu uliosainiwa mwaka huu kati ya Mbao FC na GF Truck.

 

KLABU ya Mbao ya jijini Mwanza imekabidhiwa basi lenye thamani ya Sh70 milioni kwa ajili ya wachezaji. Basi hilo wamekabidhiwa leo Jumatano na wadhamini wao Kampuni ya GF Truck and Equipments katika makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Vingunguti, Dar es Salaam.

…Akilikagua basi hilo.

Mbao inashika nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi sita, huku Simba ikiwa kileleni  na pointi 12 ikifuatiwa na Yanga ambayo ndiyo mabingwa watetezi wakiwa na tofauti katika mabao ya kufunga na kufungwa.

Mwenyekiti wa Mbao FC, Solly Njashi (kushoto) akipongezana na Mkurugenzi wa GF Trucks, Alijawad Karmali, baada ya makabidhiano.

Mkurugenzi wa GF, Alijawad Karmali, alisema basi hilo ni sehemu ya mkataba ambao waliingia na Mbao miezi miwili iliyopita. Mbunge wa Nyamagana, Angelina Mabula, ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo na aliishukuru Kampuni ya GF Trucks kwa kutimiza ahadi yao kwa Mbao.

Viongozi wa Mbao FC, Waziri Mabula, viongozi na wafanyakazi wa GF Trucks wakiwa katika picha ya pamoja baada ya makabidhiano.

Mabula ambaye ni Naibu Waziri wa Ardhi,  Maendeleo ya Nyumba na Makazi, alisema baada ya kuingia mkataba na kampuni hiyo wameanzisha kampeni ya ubingwa ili kulitoa taji kwa timu za Mkoa wa Dar es Salaam.

Basi lililokabidhiwa kwa Mbao FC.

Mwenyekiti wa Mbao FC, Solly Njashi,  alisema wanawashukuru GF  kwa udhamini huo mkubwa waliouweka kwani mpaka basi hilo wanalipokea katika mikono yao limezidi thamani ya Sh70 milioni, kwani wamelipokea likiwa limelipiwa kila kitu.

(PICHA: MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS)

 

Leave A Reply