Mbeya City Wajifua Kuwakabili Simba Kesho
- Kocha Mkuu wa Mbeya City, raia wa Burundi, Nsanzulwimo Ramadhani akiendelea kuwapa mazoezi wachezaji wake.
KLABU ya Mbeya City ya jijini Mbeya mapema leo imejinoa katika Uwanja wa Sokoine jijini humo, tayari kwa kumuwinda Mnyama Simba katika mchezo wao wa Ligi Kuu Bara, utakaochezwa kesho mjini.
Akizungumza na mwandishi wetu baada ya kumaliza mazoezi, Kocha Mkuu wa Mbeya City ambaye ni raia wa Burundi, Nsanzulwimo Ramadhani alisema, wapo kamili kumuwinda Mnyama Simba ingawa wana pengo la kipa wao raia wa Malawi, Owen Chaima aliyefungiwa na TFF.
Stori: Musa Mateja | Mbeya – Global Publishers