The House of Favourite Newspapers

Mbunge kingu aeleza sababu ya kukataa posho za bunge

0

3.Elibariki Kingu akitoa ufafanuzi wa jambo mara baada ya kuulizwa maswali kutoka kwa wanahabari.Elibariki Kingu akitoa ufafanuzi wa jambo mara baada ya kuulizwa maswali kutoka kwa wanahabari.1. Kutoka kushoto ni aliyekuwa Mgombea wa Jimbo hilo la Singida Magharibi baada ya kushindwa kura za maoni na kumuunga mkono, Hamis Ngila, Elibariki Kingu na Gerard Lukas.Kutoka kushoto ni Hamisi Ngila, aliyekuwa mpinzani wa Kingu katika kura za maoni ndani ya CCM, Elibariki Kingu na Gerard Lukas.
4.Elibariki akisoma taarifa yake aliyokuwa ameiandaa kwa wanahabari.Elibariki akisoma taarifa yake aliyokuwa ameiandaa kwa wanahabari.2.Wanahabri wakichukua tukio.Wanahabari wakichukua tukio.

MBUNGE wa Singida Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Elibariki Kingu amesema sababu za kuandika barua kwa Katibu wa Bunge kusimamisha posho zake zote za vikao ’sitting allowance’ ni kutaka fedha hizo kupelekwa kwenye mfuko wa jimbo lake kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Akizungumza na wanahabari leo katika hoteli ya Travertine jijini Dar es Salaam, Kingu amesema dhamana aliyopewa si kwa vile yeye ni bora kuliko aliochuana nao, bali ni matumaini makubwa ya wapigakura wake kwake.

Alisema wapiga kura wake wana kero kama huduma za maji, afya, ujenzi wa vyumba vya madarasa na uboreshaji wa miundombinu ya mawasiliano.

Ni kwa ajili hiyo, alisema anajiona ana dhamana na deni la kuhakikisha utekelezaji wa utatuzi wa kero hizo jimboni kwake.

Amefafanua kuwa ili aweze kuikemea serikali katika matumizi yasiyo ya lazima, ni vyema yeye kama Mbunge akatae kuchukua malipo ya vikao vya bunge kwa kipindi chake chote cha miaka mitano.

Alisema licha ya kutambua kuwa fedha hizo zipo kikanuni, alisema zitatolewa kupitia akaunti maalum ya mfuko wa jimbo lake utakaokuwa na usimamizi wa watu saba, aliowataja kuwa ni Mkuu wa Wilaya, Shekhe wa Wilaya ya Ikungi, Mchungaji wa Kanisa la SDA, Mchungaji wa kanisa la CCT, Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste, Padre mmoja kutoka Kanisa Katoliki na Afisa mipango wa wilaya.

Tayari katika siku chache ambazo amekaa bungeni kuapishwa, amesema posho yake imenunua mifuko 100 ya saruji, ikiwa ni hatua ya kwanza ya utekelezaji wake wa ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Mpetu kata ya Muhintiri.

Alisema kitendo chake cha kutochukua posho hizo ni changamoto kwa wabunge wenzake, akisema hawana sababu ya kuchukua posho ya vikao kwa vile ni kazi yao wanayolipwa mishahara.

“Ninaomba niwape mchanganuo mdogo, kama jambo hili la kukataa posho za vikao litatekelezwa ipasavyo na kupelekwa katika huduma muhimu za kijamii, kuna wabunge 394 na vikao kisheria ni siku 182, wabunge tunalipwa shilingi 220,000 kushiriki kikao cha siku moja.

“Fedha hizi kama zitaondolewa au wabunge wenzangu wataridhia kutokuchukua, basi tutakuwa tumeokoa zaidi ya shilingi bilioni kumi na tano milioni mia saba sabini na tano kwa muda wa mwaka mmoja,” amesema Kingu.

Kuhusu hotuba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli, Kingu amesema anaunga mkono kwa kufuta safari za nje kwani hatua hiyo italeta nidhamu ya uwajibikaji katika maeneo mbalimbali ya kazi na kuwapata wafanya kazi halisi watakaoweza kuifikisha Tanzania katika kuwa nchi ya asali na maziwa.

(NA DENIS MTIMA/GPL)

Leave A Reply