Mbwana Samatta alivyopokelewa leo jijini Dar
Mwanasoka Bora wa Afrika, Mtanzania, Mbwana Samatta akikatisha katika jiji la Dar leo kuanzia Hoteli ya Hyatt Regency Kempinsk mpaka Escape One akiwa katika gari la waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye (kushoto mwenye tuzo) akiwa na Mbwana Samatta.
…Akiendelea kuwasalimia wakazi wa jiji la Dar.
Madereva bodaboda walikuwa kivutio wakimsindikiza Samatta.
…Akiendelea kuwasalimia wananchi mbalimbali.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye akiongea na wanahabari.
Nape Nnauye akiongozana na Mbwana Samatta kuingia Ukumbi wa Escape One Mikocheni jijini Dar.
Makamu wa Rais wa Simba Geofrey Kaburu(kulia) akisalimiana na Samatta.
Samatta akiwa na marafiki zake katika Ukumbi wa Escape One.
Mchezaji Bora Afrika, Mbwana Samatta leo alizunguuka mitaa ya jiji la Dar kuanzia Hoteli ya Hyatt Regency Kempinsk kupitia samora, shule ya uhuru pale karume msafara ukapinda kawawa road mpaka Morocco ulipopinda tena Alli Hassan Mwinyi, mpaka njia panda ya Kawe Pale Lugalo na kuelekea Old Bagamoyo mpaka Escape One ambapo kulikuwa na hafla fupi ya kumpongeza.
PICHA: RICGARD BUKOS/GPL
Hongera sana Kijana, umewafungulia wengine njia