Mbwana Samatta atua kwa kishindo Dar
Mshambuliaji Mbwana Ally Samatta wa Tanzania na klabu ya TP Mazembe akionyesha tuzo yake ya Mchezaji Bora anayecheza soka barani Afrika baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere usiku wa kuamkia leo akitokea mjini Abuja, Nigeria.
Mbwana Samatta akipiga picha na mashabiki wake.
Baba mzazi wa Samatta, Ally Pazi Samatta (wa pili kutoka kushoto), akiwa na mke wake (wa pili kutoka kulia).
Samatta akiongea na mashabiki mbalimbali uwanjani.
Waandishi wa habari wakifanya mahojiano na Mbwana Samatta.
Mashabiki wakiendelea na shangwe baada ya kumpokea.Samatta akiondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Waandishi wa habari wakifanya yao kabla ya kuwasili Mbwana Sammata.
Mashabiki wakijiachia kwa furaha.
PICHA: RICHARD BUKOS/GPL