Mechi ya Namungo na Waangola Yafutwa
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeufuta mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya CD de Agosto ya Angola dhidi ya Namungo FC ya Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka nchini (TFF), sababu za kufutwa mchezo huo ni taratibu za #COVID19 ambapo mamlaka za Angola ziliutaka msafara wa timu yote ya Namungo kuwekwa karantini mara baada ya kuwasili nchini humo.
Suala kuhusu mechi hiyo litafikishwa katika kamati husika ya CAF kwaajili ya uamuzi.