Wakati Mashabiki na wapenzi wa mpira wa miguu Tanzania wakimiminika katika uwanja wa Benjamin Mkapa kushuhudia mechi ya watani wa jadi Simba na yanga wakipambana katika mchezo wa ngao ya Jamii, Timu ya masoko ya Global Publishers kupitia Gazeti lake pendwa la michezo la Champion imefika mapema katika Uwanja wa Mkapa kukutana na wasomaji wake pamoja na kunadi gazeti hilo .
Mkuu wa kitengo Cha Masoko Global Publishers, Juma Johanes amesema lengo kubwa ni kukutana na wasomaji wa magazeti yetu ili kutengeza ukaribu zaidi na kuhakikisha magazeti yanawafikia kila mahali popote nchini.
“Sisi Kama Kampuni ya Global Publishers tunawahakikishia wasomaji wetu wa magazeti yote ya michezo, Championi na SpotiXtra kuwa tupo imara na tutaendelea kuwapa uhondo wa habari zote za michezo kwa wakati kutoka ndani na Duniani kote”alisema Juma Johanes.