The House of Favourite Newspapers

MELI YA JESHI LA CHINA KUTOA MATIBABU NCHINI

0
Meli ya Jeshi la Maji la China ikiwa bandarini Dar es Salaam.
Makonda akipita mbele ya wanajeshi wa China waliokuja na meli hiyo.
…Akionyeshwa baadhi ya mitambo yenye kutumika katika matibabu.
Kiongozi wa msafara wa meli hiyo (kushoto) akibadilishana neno na Makonda.
…Akisaini kitabu cha wageni melini humo.
…Akiwa na viongozi mbalimbali wa meli hiyo baada ya kutembelea sehemu za matibabu.

 

MELI ya jeshi la majini kutoka China (Navy) na ambayo ni ya pili kwa ukubwa duniani,   imeingia nchini ili kutoa matibabu ya bure kwa  siku tano kuanzia kesho hadi Ijumaa Novemba 24 mwaka huu.

 

Akizungumza na wanahabari baada ya kutembelea meli hiyo na kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa ndani yake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amelipongeza jeshi hilo  kwa kuiletea Tanzania huduma hiyo bora na ya bure.

 

Alisema hayo yote ni matokeo ya ushirikiano baina ya  nchi hizi mbili ulioanza muda mrefu na jeshi hilo ni miongoni mwa taasisi zinazoendelea kuuimarisha.

 

Makonda amewataka Watanzania kufika kwenye meli hiyo kuanzia kesho ili waweze kunufaika na matibabu ya bure hasa wale wanaosumbuliwa na magonjwa sugu, yenye kuwaletea matatizo kila mara na mengine yanayowasibu.

 

NA DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply