The House of Favourite Newspapers

Messi, Suarez Waitungua Atletico, Griezman Hoi

Barcelona wameifunga Atletico Madrid katika mzunguko wa kwanza wa nusu fainali ya kombe la Copa del Rey katika dimba la Vicente Calderon.

Katika mchezo huo ulioisha kwa Atletico Madrid kuchapwa 2-1 huku magoli ya Barcelona yakifungwa na Messi pamoja na Suarez na lile la Atletico likipachikwa na Griezman, ilishuhudiwa Messi akifikisha magoli 200 katika michezo 274 ya ugenini.

Mchezo wa marudiano utakuwa Februari 7 ambapo Barcelona itakuwa katika dimba lake la nyumbani Camp Nou.

Alaves na Celta Vigo ni timu nyingine ambazo zitacheza nusu fainali Februari 8.

Save

Save

Comments are closed.