Mfanyabiashara maarufu katika visiwa vya Pemba na Unguja, Said Nasser Nassor ‘Bopar’ hivi karibuni alikuwa akitoa misaada ya tende kwa baadhi ya wakazi wa Unguja nje ya ofisi yake iliyopo maeneo ya Mombasa visiwani humo.
Mfanyabiashara huyo ambaye mara nyingi amekuwa na kawaida ya kutoa misaada mbalimbali wakati wa ramadhani na siku nyingine alisema kuwa kufanya hivyo si kwamba ni utajiri bali moyo.