The House of Favourite Newspapers

Mikopo kwa Watakaooana

0
 
Mtia nia wa kugombea urais nchini Kenya ameahidi kutoa mikopo yenye thamani ya kati ya TZS milioni 10 hadi TZS milioni 20 kwa wanandoa wapya endapo atachaguliwa katika ofisi hiyo ya juu zaidi nchini humo.
 
Aidha, amesema kuwa serikali yake itaelekeza kwamba upandaji miti uchukuliwe kama sehemu ya mahari. “Unapokwenda kulipa mahari, utatakiwa kusema na idadi ya miti uliyopanda.”
 
Gavana wa Machako, Alfred Mutua amesema hayo wakati akizindua ilani yake ya uchaguzi na kusema mikopo hiyo ya riba nafuu italipwa ndani ya miaka 20, na kwamba itawezesha wanandoa wapya kuanza maisha kwa wepesi.

Lakini ahadi hii imeibua shutuma kali na kejeli kutoka kwa Wakenya mtandaoni. Takriban wanasiasa 12 tayari wameanza kampeni za kumrithi Rais aliye madarakani Uhuru Kenyatta, ambaye yuko katika miezi ya mwisho ya miaka 10 madarakani.

Miongoni mwa wanaowania nafasi hiyo ni kiongozi mkongwe wa upinzani Raila Odinga na Naibu Rais wa sasa William Ruto, ambao wanaonekana kuwa wagombea wakuu katika uchaguzi wa Agosti 2022.

Uchumi, ukosefu wa ajira kwa vijana na kupambana na ufisadi vimeibuka kuwa masuala muhimu katika ajenda za wanaowania urais, lakini chaguzi zilizopita zimeonesha kuwa Wakenya wengi hupiga kura kwa kuzingatia ukabila badala ya masuala ya sera.

Leave A Reply