The House of Favourite Newspapers

Mjukuu Amkatakata Bibi Yake Kwa Shoka Na Kumuua-Video

0

Kijana mwenye matatizo ya akili, Steve Olumbe amemvamia, kumkatakata kwa mapanga na shoka kisha kumuua bibi yake, Priscilla Were mwenye umri wa miaka 70, katika tukio lililotokea Desemba 7, 2021 katika Kijiji cha Ruga, Kaunti ya Homabay nchini Kenya.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, kijana huyo ambaye alikuwa akiishi na bibi yake huyo tangu akiwa mdogo baada ya mama yake kufariki, alifunga kwa ndani mlango wa chumba alichokuwa akiishi bibi yake kisha kumkata kwa panga, alipodondoka chini ndipo alipommalizia kwa kumkata na shoka.

Leave A Reply