The House of Favourite Newspapers

Mkude Aanza Kujiandaa Kuondoka Simba

0
Jonas Mkude

KUFUATIA kauli ya mwenyekiti wa zamani wa Simba, Ismail Aden Rage aliyesema Jonas Mkude anapaswa kucheza TP Mazembe au Raja Casablanca ya Morocco, kiungo huyo amesema sasa anaanza kujiandaa kuondoka klabuni hapo.

Rage mapema wiki hii, aliliambia gazeti hili kwamba, Mkude ana kiwango kikubwa hivyo anapaswa kuchezea moja kati ya timu kubwa za Afrika hata TP Mazembe ya DR Congo au Raja Casablanca.

Alisema Mkude ni mmoja wa wachezaji wenye uwezo Simba ambaye amekuwa akimtabiria kufika mbali zaidi iwapo atajituma zaidi ili kuweza kucheza nje.

Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android ===>Google Play

iOS ===>Apple Store

Akizungumza na Championi Jumamosi, Mkude alisema kauli hiyo ya Rage imemzindua na sasa anapambana kufa na kupona aweze kupata nafasi ya kwenda kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.

“Rage alikuwa mwenyekiti wangu kwa muda wa miaka minne, hivyo ananifahamu vizuri kiwango changu, tena zaidi ya sana, tangu alipokuwa akiongoza.

“Amenipa hamasa kubwa ya kuweza kujituma na kupambana niweze kufanya vizuri kwa ajili yangu, familia yangu na kwake pia, nimeupokea ushauri wake kwa mikono miwili na ninashukuru kwa kunikumbusha.

“Ninajituma zaidi ikiwa ni sehemu ya kujiandaa kuondoka Simba kwenda nje ya nchi kucheza soka la kulipwa na naamini nitatimiza ndoto zangu hizi, naomba Mungu anisaidie,” alisema Mkude.

Mwanzoni mwa msimu huu, Mkude alisaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba baada ya ule wa awali kuisha.

Stori: Khadija Mngwai, Dar es Salaam

Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android ===>Google Play

iOS ===>Apple Store

Leave A Reply